Jumamosi, 7 Desemba 2013

Kilimanjaro Stars na Uganda the Cranes Kufungua mechi za robo fainali Cecafa leo

Kilimanjaro Stars na Uganda the Cranes Kufungua mechi za robo fainali Cecafa leo


DSC_0899
ROBO Fainali za kwanza za Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, Cecafa Chalenge zinatarajiwa kuchezwa leo Uwanja wa Manispaa, Mombasa, Kenya.
Mchezo unaotarajiwa kuvuta na kuteka hisia za watu wengi ni kati ya mabingwa watetezi, Uganda The Cranes dhidi ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars itakayoanza kuchezwa saa 8:00 mchana, na kufuatiwa mechi nyingine kati ya Kenya na Rwanda saa 10:00 jioni.
Uganda-Cranes
Kilimanjaro Stars wanaingia kukutana  na The Cranes inayofundishwa na kocha Mserbia Milutin Sredojevic ‘Micho’,kwenye kumbukumbu Timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars yenye idadi kubwa ya wachezaji wa Bara ilifungwa nyumbani na ugenini na Uganda katika mechi za kuwania tiketi ya kucheza Fainali za CHAN.
Kwa Uganda inaonyesha kuwa mbali zaidi hasa katika Challenge ya mwaka huu baada ya kufuzu Robo Fainali kwa kushinda mechi zake zote za Kundi C, wakati Kilimanjaro Stars ilipata ushindi  wa goli 1-0 mara mbili na sare moja hivyo kushika nafasi ya pili Kundi B.
Kocha Mdenmark, Kim Poulsen amesema kwamba anawaheshimu Uganda ni timu nzuri na anatarajia mchezo utakuwa mgumu, lakini yeye amewaandaa vyema vijana wake kushinda mechi ya leo.
Micho pia amesema Stars ni wazuri hasa baada ya kuwasili kwa washambuliaji wa TP Mazembe ya DRC, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu ambao amesema wakiungana na Mrisho Ngassa watetengeneza safu kali ya ushambuliaji.
Kwa ujumla makocha wote wanaogopana kwenye mchezo huu wa leo jambo ambalo linaashiria mechi hii kuwa kali na isiyotabirika hata chembe.
Safu ya ushambuliaji ya Stars leo inatarajiwa kuongozwa na Ngassa, Ulimwengu na Samatta wakati viungo wanaweza kuwa Frank Domayo, Salum Abubakar ‘Sure Boy’ na Athumani Iddi ‘Chuji’.
Langoni atakua ni Ivo Mapunda, kulia Himid Mao, kushoto Erasto Nyoni na katikati Said Morad na Kevin Yondan.
Kwa upande wa mabingwa watetezi, Uganda, Emanuel Okwi, Hamisi Kiiza na Dani Sserunkuma wanatarajiwa kuongoza safu ya ushambuliaji, wakati wengine kikosini watakuwa Nico Wadada, Godfrey Kizito, Khalid Aucho, Brian Majwega, Vincent Kayizzi, Godfrey Walusimbi, Savio Kabugo na Benjamin Ochan langoni.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni