Hii ni taarifa ya Polisi baada ya ofisi za Chadema kuchomwa moto Arusha.
Jeshi la Polisi Arusha limetoa ripoti kuhusu tukio la
kuchomwa moto kwa ofisi ya chama cha Demokrasia na Mandeleo Chadema kwa
kusema ‘tarehe 03/12/2013 saa 5:00 asubuhi polisi tulipokea
taarifa juu ya kuchomwa moto kwa jengo ambalo lina ofisi za Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) zilizopo mtaa wa Ngarenaro,
Halmashauri ya jiji la Arusha ambapo Askari walikwenda katika eneo la
tukio na kukuta moto umezimika’
Taarifa imeendelea kusema >> Jengo hilo ambalo lina uzio
mrefu wa matofali na geti moja la mbele lina ofisi tatu za chama hicho
ambazo ni ofisi za wilaya, mkoa na Kanda ya Kaskazini ambazo zinatumia
bafu na choo kimoja.
Uchunguzi uliofanywa na polisi kwa kushirikiana na idara ya zimamoto umegundua mambo yafuatayo:-
- Kwanza, ofisi hizo zinalindwa na walinzi wa chama hicho “red brigades” na siku ya tukio mlinzi aliyekuwa zamu alikuwa Kitumbwizi s/o Bahati (42) mkazi wa Olasiti ambaye aliingia kazini tarehe 02/12/2013 muda wa saa 12:00 jioni na kutoka tarehe 03/12/2013 muda wa saa 12:00 asubuh, ofisi hizo pia zina katibu muhtasi mmoja aitwaye Jenifer d/o Mwasha (25) mkazi wa Sombetini ambaye uwa anaingia kazini saa 1:30 asubuhi kila siku lakini siku ya tukio aliingia saa 4:00 asubuhi.
- Pili, uchunguzi umeendelea kubaini kuwa, hakuna mahali palipovunjwa kutoka kwenye uzio wa ofisi hizo kuruhusu mtu/watu kuingia ndani.
- Tatu, mlango wa nyuma wa ofisi hizo katika veranda kuligundulika tundu katika dari kuelekea bafuni tundu lenye upana wa futi moja na nusu kwa nusu (11/2×1/2) ambalo ni dogo kiasi cha kutowezesha mtu kupenya kuingia ndani ya ofisi hizo.
- Nne, ndani ya bafu kulipatikana majivu na kwenye sakafu na juu ya sinki yakiwa makavu bila maji maji yoyote.
- Tano, kuta zote za bafu na choo hazikuwa zimeungua.
- Sita, eneo lililoungua kwenye dari ni 3/4 (robo tatu mita) lenye upana wa mita 1 kwa urefu wa mita 3.
- Saba, eneo ambalo moto ulionekana umewaka, mbao katika dari zilionekana kuungua upande wa chini na upande wa juu wa mbao na ceiling board hazijaungua kuonyesha moto ulianzia chini.
- Nane, kumepatikana kipande cha chuma kilichokuwa na karatasi zilizoungua pamoja na tochi ndani ya dari eneo ambalo moto ulikuwa ukiwaka lakini vitu hivyo havikuonyesha dalili za kuungua au kushika moto na inaonyesha vimewekwa baada ya moto kuzimwa.
- Tisa, kuna uwezekano mkubwa moto huo ulizimwa kwa kutumia hewa chafu/co2.
Hii ni taarifa iliyotolewa na kaimu kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Kamishna msaidizi wa Polisi (ACP_ Japhe
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni