Yanga kwenda Uturuki Alhamisi
Wakati, Yanga wakipanga kuondoka nchini Alhamisi kuelekea
Uturuki, kiungo mchezeshaji wa timu hiyo, Athuman Idd Chuji amekalia
‘kuti kavu’ endapo atashindwa kuomba radhi kabla ya safari hiyo.
![]() |
Kikosi Cha Yanga |
Yanga imepanga kukaa wiki mbili nchini Uturuki
huku ikiwa na mipango ya kucheza mechi kadhaa za kirafiki kujiandaa kwa
ajili ya Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Michuano ya Ligi ya Mabingwa
Afrika na Kombe la Kagame.
Katika safari hiyo, Yanga imeazimia kuondoka na
wachezaji wote isipokuwa Chuji ambaye amesimamishwa kwa muda
usiojulikana kutokana na utovu wa nidhamu ambao anadaiwa kuufanya
wakati wa mechi ya Nani Mtani Jembe kwa kucheza chini ya kiwango na
hata baada ya kutolewa kuendelea kipindi cha pili, aliamua kuondoka
kabisa katika chumba cha kubadilishia nguo na kutokomea zake.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni